Sakata la CITY water
Nakuambia mambo yameiva. Hawa jamaa wa city water nani kakuambia watakubali kirahisi? Wamesema wataenda mahakamani. Nakuhakikishia hii mambo itakuwa kama yale ya TTCL. Si mnakumbuka ilianza hivi hivi kama utani. Jamaa wakagoma kutoa pesa zilizobaki. Songombingo za kisheria zikaanza. Jamaa wakavimba mahakama zote mpaka ughaibuni wakaibuka washindi. Sasa hivi wanajimwaga bado. Nasikia wataongezewa tena mkataba. Nakuapia wadanganyika tutakoma kipindi hiki. Unajua kuna watu ukiwaambia kuna wazungu matapeli watakumaliza. Watakuambia hapana, mzungu hawezi kuwa tapeli, atakuwaje tapeli wakati wao ndio magwiji na wapiga debe wa utawala bora? Hapo ndio tunapodanganywa. Tusipojihadhari tutapigwa bao lingine.