Monday, March 09, 2009

Wikipedia- Kiswahili

_Watanzania wote wanakaribishwa kuchangia habari za mahali
wanapoishi au wanapotoka katika wikipedia ya Kiswahili! (sw.wikipedia.com) Ijulikane ya
kwamba wikipedia ni mradi mkubwa wa elimu unaojengwa na wachangiaji
wanaojitolea bila malipo yoyote. Kila mtu anakaribishwa kuchangia!

Kwa sasa tumeanzisha makala fupi za kila kata kwenye mikoa ya Arusha,
Dar es Salaam, Dodoma, Iringa, Kilimanjaro, Kigoma, Lindi, Mara, Mwanza,
Mbeya, Manyara, Morogoro, Mtwara, Pwani na Tanga.

Angalia ukienda anwani hii: sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa_wa_Arusha.

Chini kuna sanduku inayoonyesha mikoa yote. Ukiingia katika mkoa fulani unapata majina ya
wilaya. Kila safari ukibonyeza kwenye neno lenye rangi ya buluu
unapelekwa kwenye makala mpya. Ukifika kwenye wilaya utaona sanduku
lenye majina ya kata za eneo hili. Makala mengi yana habari fupi tu kama
"ABC ni kata ya wilaya DEF katika Mkoa wa XYZ. Idadi ya wakazi wake
ilihesabiwa kuwa xxxxx katika sensa ya 2002". Kila mtu yuko huru
kubonyeza kwenye sehemu ya "hariri" juu ya makala na kuongeza habari.
Baada ya kuongeza habari unabonyeza sehemu ya "Hifadhi ukurasa" iliyoko
chini.

Si vigumu na hapa unaweza kuingiza habari juu ya watu, historia,
utamaduni na taasisi zilizopo katika eneo la kata hii.

Karibuni sana tutawaarifu wakati mikoa mingine itakuwa tayari!

KITABU CHA WAGENI