Wednesday, November 23, 2005

Bendera ya Uingereza yafanyani katika tovuti ya CHADEMA?

Ndesanjo amekuwa akipigia kelele matumizi ya lugha ya kiingereza katika tovuti za kitanzania. Sasa leo katika kuipitia tovuti ya CHADEMA nimeona wameweka bendera ya Uingereza juu kabisa kwenye tovuti yao. Hiyo bendera inafanya nini hapo? Mimi sijuhi sababu labda kama kuna anayefahamu anisaidie.

Tuesday, November 22, 2005

UKIMWI bado ni tishio

Shirika la umoja wa mataifa linaloshughulikia UKIMWI, UNAIDS kwa kushirikiana na Shirika la Afya duniani, WHO limetoa taarifa ya mwaka inayoonyesha jinsi UKIMWI ulivyo bado ni tishio hasa Afrika kusini mwa jangwa la Sahara. Unaweza kuisoma taarifa hiyo kwa kubonyeza hapa

Friday, November 18, 2005

Kiswahili kitolewe utumwani kwanza

Jeff Msangi kaanzisha mjadala wa kiswahili katika blogu yake. Ametoa hoja za msingi ambazo zaweza kujadiliwa. Ili mjadala ule unoge naongezea makala iliyoandikwa na Prudence Karugendo anayetoa hoja kwamba tuanze kukitoa kiswahili utumwani kwanza. Hoja yake ni kwamba kiswahili kimeazima maneno mengi sana ya kiarabu wakati tuna lugha kwa mamia za kibantu ambazo tungeweza kutumia maneno yake na kubadilisha mengi ya kiarabu. Soma makala yake hapa na mjadala uendelee.

Uvutaji na unywaji wa pombe na Saratani tena

Engidio amesema kwamba kuna watu wametishwa sana na habari niliyoiweka hapa kuhusu unywaji pombe na Saratani. Sasa naweka kiungo kingine kuonyesha msisitizo wa jambo hili tena. Soma Hapa uone mambo zaidi kuhusu pombe sigara na saratani.

Wednesday, November 16, 2005

Saratani yazidi kuongezeka shauri ya kubwia pombe

Soma habari hii inayotoa onyo juu ya ongezeko la saratani kutokana na kunywa kupindukia. Bonyeza hapa

Tuesday, November 15, 2005

Uhuru si urithi

Nimekutana na nukuu hii:

"No people are really free until they become the instrument of their own liberation. Freedom is not a legacy that is bequeathed from one generation to another. Each generation must take and maintain its freedom with its own hands." By John Henrik Clarke

Kila kizazi inabidi kipambane kujipatia uhuru wake.

Sunday, November 13, 2005

Makala za Prudence

Mzalendo mmoja aitwaye Prudence Karugendo amenitumia makala zake ambazo angependa zisomwe na watanzania wengine ili kubadilishana mawazo na kuleta changamoto katika kujadili mustakabali wa nchi yetu. Nimeweka kona ya makala zake kwenye blogu hii chini ya Kona ya Padre Karugendo. Hawa ni watu wawili tofauti. Mmoja ni Privatus mwingine ni Prudence. Kwa leo naweka makala zake tatu. Moja inaitwa kiini macho cha kusamehewa madeni. Pamoja na mambo mengine anaongelea misamiati migumu inayotumiwa katika kuandika mambo ya kiuchumi. Anahoji pia kwa nini tunaambiwa sasa tusherehekee kusamehewa madeni wakati ambao hatukuambiwa yalikopwa lini, na nani, kwa ruhusa ya nani na yalifanyia nini? Isome hapa. Nyingine mbili zinahusu amani. Moja anauliza kama kweli Tanzania kuna amani au ni kiini macho cha amani. Isome kwa kubofya hapa. Nyingine anauliza je ni upinzania au chama twawala kinachohatarisha amani? Isome hapa

Friday, November 11, 2005

Tanzania yaingizwa kwenye kapu la Misaada mingine ya Marekani

Tanzania imefanikiwa kuingizwa katika mpango wa misaada wa Marekani unaoitwa Millenium Challenge Corporation (MCC). Ili uingizwe humo ni lazima kwanza uwe na utawala bora kwa vigezo vya jamaa wa Benki ya Dunia na Wizara ya Fedha ya Dunia (International Ministry of Finance), wenyewe wanaita International Monetary Fund. Sasa tungoje majivuno na matusi toka kwa mwenyewe. "Wale wote mnaosema nchi haina utawala bora ni vipofu. Hamuoni hata Marekani inatambua? Nyie watanzania msioona ni watu wa ajabu sana". Tutayasikia haya karibuni. Soma Hapa habari hiyo.

Wednesday, November 09, 2005

Wanywaji wa Kahawa Huree

Tafiti zinachanganya Kweli. Tofauti na inavyoaminika kwamba kunywa kahawa kwa wingi husababisha Magonjwa ya moyo, utafiti mpya umegundua kwamba unywaji wa Coca Cola unaweza kuwa hatari zaidi. Soma hapa

Makala kuhusu Askari kuwachapa Raia

Bwana Sakito Mallya ameandika maoni yake kuhusu Askari wa Tanzania kuwapa kipigo raia. Makala hiyo ilitoka kwenye Gazeti la Rai la tarehe 3/11/2005. Unaweza kuisoma kwa kubonyeza hapa

Monday, November 07, 2005

Mabaki ya kanisa la kale yagunduliwa.

Jamaa mmoja kagundua mabaki ya kanisa ambalo pengine lilijengwa kwenye karne ya tatu au ya nne katika nchi "Takatifu"-Israel. Jamaa wanasemakwamba itavutia sana utalii shauri ya imani waliyo nayo wakristo kuhusu Kanisa, Yesu na nchi Takatifu. Wanabashiri kwamba utalii utaongezeka kwa nguvu sana. Hata kama jamaa wamedanganya ili kukuza sekta ya utalii bado watapata tuu. Soma habari hiyo hapa

Weusi hawasomi

Nimekutana na haya maneno katika mlolongo mmoja wa barua pepe. Soma uone jinsi weusi watakavyoendelea kunyonywa. Ina maana hata hii hawataisoma.
BLACKS DON'T READ

I think that will interest youREAD AND WEEP!BLACKS DON'T READ.Please Note:For those of you who heard it, this is the article DeeLee was reading this morning on a New York radiostation. For those of you who didn't hear it, this isvery deep and true! BLACKS DON'T READ. This is a heavypiece and a Caucasian wrote it. THEY ARE STILL OURSLAVES we can continue to reap profits from the Blackswithout the effort of physical slavery. Look at thecurrent methods of containment that they use onthemselves: IGNORANCE, GREED, and SELFISHNESS. TheirIGNORANCE is the primary weapon of containment. Agreat man once said, 'The best way to hide somethingfrom Black people is to put it in a book." We now livein the Information Age. They have gained theopportunity to read any book on any subject throughthe efforts of their fight for freedom, yet theyrefuse to read. There are numerous books readilyavailable at Borders, Barnes & Noble, and Amazon.com,not to mention their own Black Bookstores that providesolid blueprints to reach economic equality (whichshould have been their fight all along), but few readconsistently, if at all. GREED is another powerfulweapon of containment. Blacks, since the abolition ofslavery, have had large amounts of money at theirdisposal. Last year they spent 10 billion dollarsduring Christmas, out of Their 450 billion dollars intotal yearly income (2.22%). Any of us can use them asour target market, for any business venture we care todream up, no matter how outlandish, they will buy intoit. Being primarily a consumer people, they functiontotally by greed. They continually want more, withlittle thought for saving or investing. They wouldrather buy some new sneaker than invest in starting abusiness. Some even neglect their children to have thelatest Tommy or FUBU, and they still think that havinga Mercedes, and a big house gives them "Status" orthat they have achieved the American Dream. They arefools! The vast majority of their people are still inpoverty because their greed holds them back fromcollectively making better communities. With the helpof BET, and the rest of their black media that oftenbroadcasts destructive images into their own homes, wewill continue to see hug profits like those of Tommyand Nike. Tommy Hilfiger has even jeered them, sayinghe doesn't want their money, and look at how the foolsspend more with him than ever before). They'llcontinue to show off to each other while we buildsolid communities with the profits from our businessesthat we market to them. SELFISHNESS, ingrained intheir minds through slavery, is one of the Major wayswe can continue to contain them. One of their own,Dubois said that there was an innate division in theirculture. A "Talented Tenth" he called it. He wascorrect in his deduction that there are segments oftheir culture that has achieved some "form" ofsuccess. However, that segment missed the fullness ofis work. They didn't read that the "Talented Tenth"was then responsible to aid the Non-Talented NinetyPercent in achieving a better life; instead, thatsegment has created another class, a Buppies classthat looks down on their people or aids them in acondescending manner. They will never achieve what wehave. Their selfishness does not allow them to be ableto work together on any project or endeavor ofsubstance. When they do get together, theirselfishness lets their egos get in the way of theirgoal. Their so-called help organizations seem to onlywant to promote their name without making any realchange in their community. They are content to sit inconferences and conventions in our hotels, and talkabout what they will do, while they award plaques tothe best speakers, not the best doers. Is there no endto their selfishness? They steadfastly refuse to seethat TOGETHER EACH ACHIEVES MORE (TEAM)! They do notunderstand that they are no better than each other ofwhat they own in fact, most of those Buppies are butone or two paychecks away from poverty. All of whichis under the control of our pens i our offices and ourrooms. Yes, we will continue to contain them as longas they refuse to read, continue to buy anything theywant, and keep thinking they are "helping" theircommunities by paying dues to organizations which dolittle other than hold lavish conventions in ourhotels. By the way, don't worry about any of themreading this letter, remember, THEY DON'T READ!!!!BLACKS DON'T READ"Euseby

Saturday, November 05, 2005

Kwa nini?

Umeshawahi kujiuliza kwa nini Amani Karume awe rais wa Zanzibar? Kwa nini Ndugu yake ni balozi? Kwa nini Hussein Mwinyi ni Naibu Waziri wa Afya? Kwa nini Watoto wawili wa Nyerere ni wabunge wa kuteuliwa? Kwa nini? Nimeulizwa. Mimi nikasema kwa vile ni wanasisiemu wazuri. Nikaulizwa je ni wao tuu ambao ni wanasisiemu wazuri? Je ni kwa vile baba zao walikuwa Rais kwa vipindi tofauti? Sijuhi.

KITABU CHA WAGENI