Sunday, November 13, 2005

Makala za Prudence

Mzalendo mmoja aitwaye Prudence Karugendo amenitumia makala zake ambazo angependa zisomwe na watanzania wengine ili kubadilishana mawazo na kuleta changamoto katika kujadili mustakabali wa nchi yetu. Nimeweka kona ya makala zake kwenye blogu hii chini ya Kona ya Padre Karugendo. Hawa ni watu wawili tofauti. Mmoja ni Privatus mwingine ni Prudence. Kwa leo naweka makala zake tatu. Moja inaitwa kiini macho cha kusamehewa madeni. Pamoja na mambo mengine anaongelea misamiati migumu inayotumiwa katika kuandika mambo ya kiuchumi. Anahoji pia kwa nini tunaambiwa sasa tusherehekee kusamehewa madeni wakati ambao hatukuambiwa yalikopwa lini, na nani, kwa ruhusa ya nani na yalifanyia nini? Isome hapa. Nyingine mbili zinahusu amani. Moja anauliza kama kweli Tanzania kuna amani au ni kiini macho cha amani. Isome kwa kubofya hapa. Nyingine anauliza je ni upinzania au chama twawala kinachohatarisha amani? Isome hapa

0Comments:

Post a Comment

<< Home

KITABU CHA WAGENI