Monday, February 09, 2009

HAKUNA APANDAYE JUU YA MTI KUTAFUTA SAMAKI!!

kooooorti!!!watu wote wanasimama kuashiria mheshiwa hakimu kashatia maguu ndani ya mjengo...prosija za mahakama zinaendelea na baada ya muda mreefu tangu 2006 hatimaye leo kile kitendawili cha KATI YA ULIMI NA MENO NANI MPANGAJI NDANI YA KINYWA kinaanza kujibiwa...najua unashauku ya kutaka kujua nazungumzia nini...Ni yule jamaa alikuwa mtu mzito ndani ya Geshi la polisi...A.Zombe...akiwa na washikadau wenzake kwa kesi ya kuua wafanyabiashara wa madini..Nimekuwa nikifuatilia kesi hii na hapa mwishoni mwakili wa Zombe wanadai mteja wao hana kesi y kujibu eti kwa sababu ushahi ulotolewa unaonyesha hakuwepo eneo la tukio..kweli kila mtu na kazi yake...ukiwa wakili lazma ukubali kuwa na uwezo wa kujipiga ganzi...Haya...Ushahidi unaonyesha kuwa order zote zilitoka kwa zombe...hapa ni kwamba hata kama hakuwepo ktk eneo bado anakesi ya kujibu..MATUMIZI MABAYA YA OFISI...na hapo ndipo napotaka kutundika mawazo yangu...kilaiini kama kuweka shati kwenye msumari...Ninaposema hakuna mtu mzima mwenye akili timamu amabye anaweza kupanda hadi juu ya mti na kisha akiulizwa anatafuta nini!?aseme" NATAFUTA SAMAKI"namaanisha kwamba Zombe na wenzake walijua dhahiri walichokuwa wanafanya..na hivyo umefika wakati wa wao kuambiwa"KWENYE MTI HUWA KUNA MATUNDA"...ili jamii yetu iweze kuwa na imani na vyombo vyake vya sheria tunategemea kuona Zombe na wenzake wakipata matunda ya kazi yao..Kwani kama Zombe ndiye mwenye nyumba basi Mahakama imtoe na kicheko..lakini kama yeye na wenzake na wapangaji ndani ya kinywa(SHERIA)basi mwenye kupewa notice apewe!!!vinginevyo itakuwa sawa na kile kitendawili cha KATI YA NGUO NA MWILI NANI ANAYEMBANA MWENZAKE???!!

KITABU CHA WAGENI