Tuesday, June 12, 2007

Askofu agawa kondomu

Alhamisi ya tarehe 7 Juni 2007, BBC ilirusha kipindi cha Hard Talk ambapo mwandishi maarufu Steven Suckur alifanya mahojiano na Askofu Mkuu wa Dayosisi ya Rusternburg Nchini Afrika ya Kusini. Askofu huyo, Kevin Dowlin alikiri kugawa kondomu kwa watu ili wajikinge na maambukizi ya UKIMWI. Alisema kwamba yeye kama askofu ameshuhudia mengi, anaona watu wakifa ambapo pengine wangestahili kupona. Alisema katika moja ya kliniki sehemu hizo, asilimia 50 ya wanawake wanaohudhuria kliniki ya wajawazito wameambukizwa virusi vya UKIMWI. Wengi wa wanaothirika ni wahamiaji masikini kutoka katika majimbo yenye hali mbaya sana kimaisha hase jimbo la Eastern Cape. Baadhi ya wahamiaji hao huja kutafuta namna ya kujikwamua kimaisha katika maeneo hayo ambapo kuna mgodi wa madini, lakini wengi hasa wanawake hujikuta wakijihusisha na ngono kama njia ya kujikimu baada ya kukuta hakuna cha kufanya.

Alipoulizwa kama haoni huku ni kupingana na Vatican, Askofu huyo ambaye pia alikuwa mmoja wa wapambanaji wa mfumo wa ubaguzi wa rangi nchini humo alisema ni kweli mtazamo wa kanisa si huo lakini yeye anaangalia hali halisi na mazingira aliyomo. Anasema akiwatembelea watu katika maeneo hayo wanaoishi kwenye vibanda vibovu kabisa anawakuta wengi wakiwa katika hali mbaya sana jambo linalomfanya ahisi kwamba wangeweza kupona kama wangejikinga. Hilo linamsukuma kuwagawia kondomu watu wengi ili kuponya maisha yao na madhara yanayoambatana na UKIMWI. Anaendelea kusema kuwa watu anaowahudumia si wakatoliki tu bali ni kutoka katika dini na madhehebu mbalimbali na kwamba anachofanya ni kujaribu kuwasaidia watu kutua mizigo na si kuwatwisha kama neno la bwana linavyonena!

4Comments:

At 7:01 PM, Anonymous Anonymous said...

ukristo uliletwa ili uwezeshe urahisi wa kutawala watu. Uislamu vilevile.
Yote yalitokea huko uyahudini. Wajeuri wote wanaamua ulimwengu uende wapi.
Kumbuka kaka wataalamu wa dunia hii ni hatari. Utadhani kuwa ubadhilifu na ufisadi wote uko hapo tza tu, lakini ukweli ni kwamba umeenea kote. Waenezao haya ni wachache tu duniani. Na haya yalianza zamani.
Ingia website hizi uone.
http://judicial-inc.biz/slave_traders_.htm,
http://judicial-inc.biz/b.lood_diamonds.htm,
http://judicial-inc.biz/J_oran_va_der_sloot_supplement.htm,
http://judicial-inc.biz/thersea_heinz_kerry_bio.htm,
http://judicial-inc.biz/1.osephardim_of_curacao.htm,
http://judicial-inc.biz/j_history_caribbean_jews.htm,
http://www.blacksandjews.com/Jews.of.Black.Holocaust.ag.html,
http://sunray22b.net/slavery.htm,
www.jewwatch.com, www.erichufschmid.net, www.iamthewitness.com, www.prothink.org.

 
At 5:49 PM, Anonymous Anonymous said...

maybe english version year 3030

Auto Parts

 
At 8:33 PM, Anonymous Vimax Canada said...

Nice blog and article, thanks for sharing. However want to statement on few common issues, The website taste is great, the articles is in point of fact excellent. visit me: Vimax pills

 
At 9:03 PM, Anonymous Vimax Canada said...

That's what everyone likes. You have a good imagination. Great post thanks you

 

Post a Comment

<< Home

KITABU CHA WAGENI