Saturday, July 29, 2006

Makala ya Karugendo Kumuaga Chachage

Padre Karugendo kaandika makala kuhusu prof. Chachage. Yeye anasema anamlaumu sana Chachage. Ni muhimu uisome ujue anamlaumu kwa nini. Naibandika hapa

Wednesday, July 19, 2006

Tenzi za Kumuaga Prof. Chachage

Prof Shivji na Jenerali Ulimwengu waliandika tenzi za kumuaga Prof. Chachage. Unaweza kusoma wa Shivji kwa kubonyeza hapa na wa Ulimwengu kwa kubonyeza hapa

Monday, July 17, 2006

Buriani Prof. Chachage

Mengi yameshaandikwa na kusemwa kuhusu Marehemu Prof. Chachage aliyetutoka hivi karibuni. Mwanazuoni huyu ambaye hakuendekeza kabisa uvivu wa kufikiri ametutoka katika kipindi ambacho kwa vyovyote watu walikuwa wakitaraji mengi toka kwake. Lakini hata hivyo katuachia mengi ya kusoma. Siku za nyuma niliuliza ni wangapi walikuwa wamesoma Makuhadi wa Soko Huria. Kitabu alichoandika Prof. Chachage mwaka 2002. Ukikisoma pamoja na vitabu vyake vingine kama Sudi ya Yohana na Almasi ya Bandia ndipo utamwelewa msimamo wake na uwezo wake wa kufikiri. Jenerali Ulimwengu na Issa Shivji wameandika tenzi kwa ajili ya kumbukumbu ya Chachage. Nitaziweka hapa ili wengi wazisome.

KITABU CHA WAGENI