Friday, April 21, 2006

Ripoti ya Transparency International kuhusu IPTL na Tanesco

Nimepata kupitia barua pepe yangu taarifa iliyotolewa na transparency international kuhusu lile dude la Tegeta linalogharimu serikali shilingi bilioni tatu kila mwezi (hapa ni wakati ambapo halijawashwa) Likianza kutoa umeme tuu unalipa bilioni tatu za kila mwezi na kulipia umeme watakaokuuzia. unaweza kuisoma hapa

Thursday, April 13, 2006

Urasimu Mpaka lini?

Kuna Mtanzania mmoja anayeishi nchini Marekani ameandika maoni kwenye blogu yangu jinsi urasimu ulivyo kwenye pasipoti mpya. Nachapisha maoni yake hapa chini. Je na wengine mmepata matatizo kama haya? Lazima nikiri kwamba mimi binafsi sikupata tatizo lolote lakini sipo Marekani. Nipo Kusini.

Urasimu mpaka marekani!! Mimi ni mgeni kwenye blog yetu hii na ni mtanzania ninayeishi marekani.Kuna jambo moja linalosumbua vichwa sana hasa kwa tuliopo huku,jambo hili ni urasimu ulikithiri kwenye ubalozi wetu wa huku.Ni swala la passport mpya ambazo tumelipishwa fedha nyingi kwa kufanya process ya kubadilisha,kuna state tumelipa karibu dollar 95(laki na upuuzi kwa fedha zetu za madafu).Toka mwezi wa sita/saba 2005 kwa malengo ya kutumiwa kwenye address zetu by sept/octoba 2005.Cha kushangaza sana ni kuwa huyu ndugu wa marehemu Sokoine alitumia nafasi hii kujitengenezea fedha kisha kuingia mitini.Kama tulilipa ghalama zote ili passport zetu zitumwe kwenye makazi yetu,inakuaje tena tunatakiwa tuzifuate washington?Waliojaribu kwenda DC walitakiwa kutoa hongo ili kupata passport zao.This is bullshit wewe bwana sokoine,tambua kuwa fedha zile watu hawakuziokota bali ni kuzifanyia kazi.Keep in your freak-ass mind,next time unakuja Kansas,tegemea kukabiliana na bakora za maana.Acha kuharibu jina la marehemu wewe,na kama ulihitaji fedha ungesema mapema tukatafuta njia ya kukusaidia.

Tuesday, April 04, 2006

Askofu akumbushwa Mwanae

Mwenye kumwandikia baruapepe hii Askofu Severini ameniambia niiweke kwenye blogu ili watu wengine wasome kwamba "Baba Askofu" ana mtoto huko Arusha.

Date:
Wed, 15 Feb 2006 02:00:45 -0800 (PST)
From:
"Antiparth Martin"
Subject:
Mkunde!
To:
niwemugizi@iwayafrica.com
CC:
nunzio@cats-net.com, nyumba@cats-net.com, tec@cats-net.com
HTML Attachment [ Download File Save to Yahoo! Briefcase ]

Mtumishi wa Mungu, Askofu Severine Niwemugizi, Askofu wa Jimbo Katoliki la Rulenge na Mwenyekiti wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania.
Tumsifu Yesu Kristu.

Mtumishi wa Mungu,
Pole sana kwa kazi nyingi ya kuchunga kondoo. Bwana akubariki na kukuzidishia moyo mkuu. Ninakuandikia ujumbe huu kukumbusha jambo moja:

Unakumbuka siku chache kabla ya kuchaguliwa kuwa Askofu wa Jimbo Katoliki la Rulenge, ulizaa mtoto na Consolata Kyala, dada yake na Padri..... wa Jimbo Kuu la Dar-es-salaam. Padri huyo alikutunzia siri, na sisi tukanyamaza! Mtoto wako Mkunde, anaendelea kukua na sasa anasoma shule Maji ya Chai Arusha.

Ili Consolata Kyala, akae kimya, ulimjengea nyumba kule Maji ya Chai Arusha. Sasa hivi anaishi kwenye nyumba hiyo na mme wake Antiparth Martin. Hapo hapo anaendesha biashara ya Bar ijulikanayo kwa jina la Holiday Inn.

Tumesikia tetesi kwamba hivi karibuni utateuliewa kuwa Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Tabora. Tunafikiri ni jambo la muhimu na la lazima, viongozi wa Kanisa kufahamu kwamba wewe una mtoto. Ofisi ya Askofu Mkuu ni kubwa na yenye kudai maadili ya Kanisa Katoliki.

Viongozi wa kanisa wanaweza kupuuzia jambo hili. Nawe pia unaweza kupuuzia jambo hili. Kwa vile siku hizi sayansi imepiga hatua, tutasisitiza ipimwe DNA yako na ya mtoto Mkunde. Tunataka watanzania wajue ukweli huu na ulimwengu ujue ukweli huu.

Ni matumwaini yetu kwamba utaupokea ujumbe huu na kuwajibika ipasavyo.
Tunakutakia moyo mkuu.

Kwa niaba ya waumini wenye upendo na kanisa katoliki wa Maji Chai-Arusha.
Ni, wako katika Upendo wa Kristu.
Antiparth Martin.

KITABU CHA WAGENI