Saturday, May 14, 2005

Baba Moi Mjanja mwenzao

Nasikia kati ya mambo ambayo rais mstaafu wa Kenya Daniel Arap Moi ameyafanya ni pamoja na kujenga chuo kikuu katika shamba lake kubwa huko Turkana. Chuo hicho kwa mujibu wa taarifa nilizonazo kina wanafunzi karibia mia tatu. Hii kwa mtazamo wangu ni kitu kizuri zaidi kuliko wanavyofanya viongozi wengi wa Afrika kuweka fedha zao katika mabenki ya Uswisi au nchi nyingine za magharibi. Angalau zikiwekezwa nchini zinaweza kufaidisha wananchi.

0Comments:

Post a Comment

<< Home

KITABU CHA WAGENI