Monday, May 09, 2005

Demokrasia na Mkumbokrasia

Hivi kweli wengi ndio Demokrasia? Nadhani kuna Demokrasia na Mkumbokrasia(Mobcracy). Kuna mtu leo ukimuuliza kwa nini anamshabikia mgombea fulani wa kiti cha urais hawezi kukupa sababu. Mwingine haelewi hata huyo anayemshabikia ana ajenda gani. Kuna msemo unazungumzwa sana sasa hivi- huyu ana mvuto. Muulize sasa mvuto kwa nini? Hapo ni heri umchape fimbo sita kuliko akupe jibu kwa sababu atakuwa hana. Kama wapiga kura wengi wanafuata mkumbo kutakuwa hakuna Demokrasia bali ni Mkumbokrasia.

1Comments:

At 4:59 AM, Anonymous Anonymous said...

Yote tisa, kumi ni hilo neno mkumbokrasia

 

Post a Comment

<< Home

KITABU CHA WAGENI