Wednesday, May 04, 2005

Kutawala kwa zamu

Kuna wakati Macha alipendekeza njia za kumpata rais. Kati ya hizo ni kuwa na rais mwislamu na Mkristo kwa sababu watu wa dini hizi mbili wameshika bango sana. Nyingine ilikuwa ni Kumomba George Kichaka atusaidie kama anavyosaidia Iraq na Afrighanistan na nyingine ambazo hazitangazwi lakini ziko chini ya uangalizi wake. Mimi napendekeza utawala kwa zamu. Kwa vile rais anaweza kuongoza kwa miaka kumi basi ni rahisi sana hawa jamaa wote waliojitokeza kupitia CCM wakaongoza kwa zamu yaani mwaka mmoja mmoja watakachokubaliana tuu ni kuondoa "Outlier". Yule wa kumi na moja aondolewe kwa kigezo cha umri. Mwenye umri kubwa aombwe akapumzike kijijini kwake kwa amani, waliobaki watawale kwa mwaka mmoja mmoja. Hii itasaidia sana "kuimarisha mshikamno" wa chama twawala. Rais akichaguliwa ahakikishe anashawishi bunge kubadili katiba ili staili hii mpya ikubalike

0Comments:

Post a Comment

<< Home

KITABU CHA WAGENI