Tuesday, May 03, 2005

Asilimia kumi, Rushwa na Sadaka

Umeshawahi kujiuliza uhusiano kati ya asilimia kumi, rushwa na sadaka? Swali hili linanitatiza sana kwani tunaambiwa Bwana Mungu wa Ibrahim, Yakobo na Isaka alisema tumtolee asilimia kumi ya pato letu. Upande mwingine tunaambiwa kwamba rushwa mara nyingi huwekwa katika kiwango cha asilimia kumi ya gharama halisi ya pato utakalopata. Kwenye mfumo wa rushwa,iIli kupata tenda tunaambiwa kwamba unahitajika uwape watoa tenda asilimia kumi. Kuna uhusiano wowote au ni hisia zangu tuu?
Sadaka mimi bado sijaweza kuielewa vizuri. Muumba wa mbingu na nchi na vyote vilivyomo anaitaji kweli visenti vyako? Kama anavihitaji basi asilimia kumi ni lazima iwe baada ya kutoa matumizi yako. Hivyo kama unapata laki moja, basi utoe kodi ya nyumba, chakula, usafiri, ada ya watoto, matibabu nakadhalika. Kitakachobaki toa asilimia kumi mpe muumba.

0Comments:

Post a Comment

<< Home

KITABU CHA WAGENI