Thursday, May 05, 2005

Ujana na Urais

Kwa kweli kabla hujafa hujaumbika. Kijana anakuwa na miaka 55? Hiyo ni kali zaidi. Naambiwa mwenyekiti wa CCM katika hotuba yake ya mkutano mkuu wa kumtafuta mgombea alitoa wito kwamba ateuliwe mtu kijana. Angetoka wapi wakati hakuwepo kijana kwenye jopo hilo? Hata lile la watu 11 hakuwepo. Kuna watu wanaosema kwamba hotuba ya Mwenyekiti huyo imemsaidia mshindi. Wenye mtazamo huo wanakubali kwamba ni KIJANA. Kijana miaka 55? Hiyo ni definition mpya sana ya CCM. Lakini imekuwepo muda mrefu sana. Sasa hivi wastani wa muda wa kuishi kwa mtanzania ni kama miaka 46 sasa hapo ina maana kwamba hata umri wa wazee na vijana upangwe upya. Hata umri wa kustaafu kazini upunguzwe pengine uwe miaka 50. Umri wa kugombea urais kikatiba inabidi upunguzwe pia. Kila kitu kinabidi kirekebishwe kulingana na umri mpya wa kuishi kwa sababu hakuna matarajio kwamba siku za karibuni wastani huo utapanda.

0Comments:

Post a Comment

<< Home

KITABU CHA WAGENI