Wednesday, May 18, 2005

Daktari azidi kubanwa

Yule Daktari mjerumani anayepinga matumizi ya dawa za makampuni ya kibeberu na kusisitiza matumizi ya vitamini amezuiwa na mahakama huko Berlin kuendelea kutangaza kwa kijerumani kwamba vitamini zake zina uwezo wa kutibu kansa la sivyo atatozwa faini ya EURO 250,000. Hatua hiyo inafuatia kugundulika kwamba kijana mmoja kwa jina la Dominik Feld mwenye umri wa miaka tisa alikufa baada ya kuanza kutumia vitamini za Dr. Rath na kusimamisha tiba ya kansa aliyokuwa akiendelea nayo. Mambo yanazidi kuwa moto. Mambo ya kufanyika maabara sasa yamegeuka ukumbi wa mabishano kama siasa. Nitazidi kuwafahamisha maendeleo ya mkasa huu.

0Comments:

Post a Comment

<< Home

KITABU CHA WAGENI