Saturday, May 14, 2005

City Water

Soma habari hii hapa uone jinsi hawa "wenzetu" wawekezaji wanavyofanya. Habari za hawa jamaa kwamba walikuwa hawana chochote zilisemwa siku nyingi sana lakini kama kawaida waliosema wakaanza kupigwa mabomu na viongozi. Wakaambiwa si wavumilivu. Wakaambiwa kampuni yenyewe ndio kwanza imeanza kazi lakini watanzania wanataka mabadiliko haraka sana. Wakaambiwa subirini. Sasa sijuhi wataombwa radhi wale waliokuwa wanasema ukweli kwamba hao jamaa hawataweza kufanya lolote au vipi? Wamesubiri na maneno yao yamethibitika. Wakati mwingine viongozi wajifunze kusikiliza pia sio kutoa maagizo na vitisho tuu kwa watu wenye mawazo na maoni tofauti.

0Comments:

Post a Comment

<< Home

KITABU CHA WAGENI