Tuesday, March 14, 2006

Mawaziri wetu

Niliposoma habari kwamba mawaziri wanalala Hotelini kwenye Blogu ya Da Mija nilitoa maoni kwamba sikushangaa kwa hilo. Sababu ya kusema hivyo ni kwamba nilitarajia. Kwa nini nisingetarajia kwa sababu nyumba zote ziliuzwa? Wakati nashangaa hilo nakutana na habari kwamba mmoja wa naibu waziri ambaye alikuwa akifanya kazi nchini Botswana kama mwalimu kwenye chuo kimoja cha kilimo na kujifanya anaumwa sana kumbe wlikwenda kwenye kampeni. Alikuwa akilipwa mshahara huku akiwa anapiga kampeni. Nimeikuta hii habari kwenye barua pepe yangu labda wengine mmeisoma lakini niiweke muione. Hii ni kashfa ya hali ya juu sana. Kingine ni kwamba huyu jamaa kuna watu wanahoji shahada yake ya PHD kaipata wapi? Kwenye maelezo yake binafsi katika tovuti ya bunge anadai Free State University. Kuna watu wamejaribu kuitafuta hii University ilipo lakini haijaonekana. Soma habari hii hapa chini:


Tanzanian minister on Botswana's payroll?
by Sarah Mophonkolo
2/14/2006 7:39:04 AM (GMT +2)
A Tanzania deputy minister may still be drawing a salary from Botswana
government almost eight months after he returned to his native country.
Authorities were this week sent in to a frenzy at the shock revelation
that Dr. David Mathayo David (37) who was employed as a lecturer in
agriculture at the Serowe College of Education, was in fact paid to
fund
his political campaigns last year. !

College Principal Caiphus Dema said they did not know that David was
involved in politics. "What we know is that he went on a three week
sick
leave last year in June. He said he wanted to be close to his family.
When the leave was over he applied for an extension a number of times
saying he was still very sick," Dema said.
A reliable source has alleged that David is still on government!
payroll. "He is still getting paid as he is still considered an
employee
of the college," she said. Nevertheless, Dema said he doubted that
David
was still getting paid. "He said he was considering resigning as he was
too sick to work," Dema said. He said when he did not return, they went
to his house sometime last year to reclaim the school furniture. "It
did
not appear as if he had left any of his belongings," Dema s! aid.

David became a Member of Parliament for Same Magharibi (West)
constituency under the ruling party, Chama Cha Mapinduzi ticket after
the October parliamentary elections. He was subsequently appointed
Deputy Minister of Industry, Trade and Marketing December 28 last year.
Approached for comment, the Teacher Service Management (TSM) referred
us to the Department of Teacher Training and Development. The Deputy
Director, Tebogo Mongatane, requested a questionnaire last week saying
she feared being misquoted. She had promised to answer the
questionnaire
as soon as it was sent. Nevertheless, a follow-up on Friday afternoon
found she had 'other important obligations.'

On Monday afternoon she sent a res! ponse advising us to "direct
these
questions to TSM, who are employer and are responsible for all
employment matters affecting teachers." Efforts to reach David for
comment proved futile.
_______________________________________________________

Comments za watu wa karibu na mweshimiwa:
Hii habari inatia woga kidogo. Ukiisoma inaonyesha Naibu Waziri sio
mkweli.

Alimdanganya mwajiri wake kuwa anaumwa kumbe yuko kwenye harakati zake
za kisiasa. Hapa kidogo panatia shaka kama hatamdanganya Mheshimiwa
Rais
kwenye wadhifa wake mpya alionao mradi mambo yamwendee.

Huyu jamaa kuna sehemu nyingine wanamjadili pia, wanasema elimu yake
iliyoonyeshwa kwenye website ya bunge sio kweli. Naanza kuamini kuwa
hata kwenye sifa zake ametia chumvi kama style yake ndio hii. Nanukuu
"Mh. Mathayo David Mathayo (naibu waziri wa biashara na viwanda),
alisoma SUA degree ya wanyama (Ba! chelor Vet. Medicine) kati ya
1992-1997 na tulikuwa tunakaa naye Hall moja pale na nilimwacha pale,
na
baaada ya hapo alifanya kazi kidogo Botswana na akarudi nyumbani
kujiunga na! NEC ya CCM (kutokea kundi la vijana), sasa cha kushangaza
hivi sasa ana PhD ambayo haijulikani kaipatia wapi na lini, mwanzo
nilifikiri wanamwita Dr . kutokana na field yake wanyama kumbe
nilipopitia CVs za wabunge, nimegundua naye kapata PhD from Free State
University(kwa kifupi hii university haipo ni feki-jaribuni ku-google
wenyewe). Tena kwa kifupi hana hata Masters degree jamani, sishangai
kupewa wizara nyeti bali kinachoikumba Kenya kipo njiani kuja Tanzania,
hii ndiyo ! labda kasi ya kundi la vijana katika kujiingiza kwenye
siasa
kwa mbwembwe za kwamba waonekane wasomi haswa"
___________________________________________________________
mmmmh!, mambo ya bongo hayo!

Monday, March 06, 2006

Kuadi wa soko huria atoswa

Waziri Mkuu wa Libya bwana Shukri Ghanem ametemwa kazi yake japokuwa alikuwa akipata umaarufu mkubwa toka sekta binafsi. Kamati inayoshughulika na sera za Serikali inasemekena kutopenda mageuzi makubwa aliyotaka kuyafanya ya kuuza kila kitu. Soma habari hiyo hapa

KITABU CHA WAGENI