Monday, March 06, 2006

Kuadi wa soko huria atoswa

Waziri Mkuu wa Libya bwana Shukri Ghanem ametemwa kazi yake japokuwa alikuwa akipata umaarufu mkubwa toka sekta binafsi. Kamati inayoshughulika na sera za Serikali inasemekena kutopenda mageuzi makubwa aliyotaka kuyafanya ya kuuza kila kitu. Soma habari hiyo hapa

9Comments:

At 10:04 AM, Blogger mwandani said...

Tusubiri vikwazo vipya vya kiuchumi kwa Libya.Wamagharibi wanaheshimu sana private property, hairuhusiwi kuzorotesha ubinafsishaji wa soko huria. Kufukuzwa kwa kuwadi huyu ni kosa ambalo walibya wote watashinikizwa kulipia.
Soko huria, ubepari tandawazi hauwezi kamwe kukubali kusitishwa jitihada zake. Libya ilikuwa imeshaanza kusamehewa baada ya kurudisha makampuni ya mafuta machache yaliyotaifishwa mwaka 67.
kuwadi aliyetayarisha mikataba hiyo kawekwa kando...
hebu tuone yanayokuja

 
At 3:08 PM, Anonymous Anonymous said...

Unaambiwa sera za Waziri Mkuu zilipendwa na wafanyabiashara na kupingwa na wakomunisti! Hii sentesi moja imejaa mengi! Je, hao wafanyabiashara wanawawakilisha na wamachinga? Na hao wakomunisti ni nani? Ni chama, kabila, NGO, dini, au ni walalahoi wanaokataa kunyonywa na wachache kwa kisingizio cha mageuzi ya biashara. Wakibinafsisha basi wawape wananchi hisa!

 
At 9:12 AM, Anonymous ndesanjo said...

Nkya, jina kuwadi ninalipenda sana. Kuwadi wa soko huria. Viongozi wetu wote Afrika ni makuwadi wakuu.

Unajua kuna mzozo marekani ambao unaonyesha jinsi gani soko huria ni sera ambayo sisi tunalazimishwa kuichukua asilimia mia ila wao hawafanyi hivyo. Kuna kampuni toka Uarabuni imepewa ruhusa ya kuendesha shughuli za bandari kadhaa, sasa wabunge wamekuja juu wanasema kwanini shughuii ya sekta muhimu kama hiyo iende kwa wageni. Umepelekwa msaada bungeni ambao utakataza kampuni za nje kuendesha shughuli za sekta nyeti. Wengne wanaanza kuhesabu makampuni ya kigeni yaliyoko marekani na kusema kuwa kuna dalili kuwa uchumi wa marekani unauzwa maana makampuni ya kigeni ni mengi. Unajiuliza: hiyo sio ndio sera ya soko huria wanayoisambaza dunia muzima?

 
At 3:31 PM, Anonymous Anonymous said...

Hiyo kampuni ya bandari inayomilikiwa na mashehe wa Dubai bwana Clinton ndiye aliyepiga pasi ya kisigino. 10 percent imeshaingia. Mkewe Clinton, Hillary
kwa kuwa anatafuta cheo cha siasa anakuja juu sana kwa nini wamanga wapewe tenda. Hivi pochi hilo hawalitumii pamoja yeye na mumewe?
- Tunga

 
At 8:03 AM, Anonymous ndesanjo said...

Nkya, umeishilia cha wapi tena?

 
At 8:35 AM, Blogger Bwaya said...

Viongozi wetu wote Afrika ni makuadi wakuu...ukweli mtupu!

 
At 12:51 PM, Blogger Indya Nkya said...

Unajua Marekani huwa inahubiri A halafu inafanya B. Kuna Profesa mmoja Mmarekani ambaye kila siku anazishahuri nchi changa kutouata ushauri wa Marekani na anadai kwamba China haina chochote cha kujifunza toka Marekani. Nitatafuta baadhi ya maandiko yake niyaweke

 
At 5:31 PM, Anonymous ndesanjo said...

Marekani ikitoa ushauri, kitu cha kwanza inachoangalia ni jinsi ambavyo ushauri huo utaisaidia Marekani zaidi ya nchi inayopewa ushauri! Nasi tulivyo tunakubali. Sijui ni ule mtazamo wa "wazungu achana nao bwana! Wana akili kweli!"

 
At 3:25 PM, Blogger mwandani said...

Nadhani profesa unayemzungumzia ni Joseph Stiglitz. Alikuwa mshauri mkuu waIMF wakati fulani, sijui vipi hawataki kabisa IMF/WB kila siku anachimbua uwongo wao.

 

Post a Comment

<< Home

KITABU CHA WAGENI