Thursday, January 19, 2006

Nawajibika kuomba Radhi

Kwa kweli nimepotea bila kutoa maelezo kwanza. Naomba radhi kwa hilo Ndesanjo kataka kuunda tume pamoja na kutaka kuwasiliana na FBI nitafutwe. Nimerudi. Naanza na nukuu hii ya Frantz Fanon. Kwamba wananchi ndio nguvu ya kubadili mambo. Niliwahi kuizungumzia bila kuiweka nukuu yenyewe: “To educate the masses politically does not mean, cannot mean making a political speech. What it means is to try, relentlessly and passionately, to teach the masses that everything depends on them; that if we stagnate, it is their responsibility and that if we go forward it is due to them too, that there is no famous man or woman who will take responsibility for everything and the magic hands are finally only the hands of the people”. Frantz Fanon
Nimeiweka ili kusisitiza kwamba tuna wajibu wa kuelimisha na kwamba sisi pia ni wananchi ambao tunaweza kuleta mabadiliko.

KITABU CHA WAGENI