Tuesday, January 03, 2006

Kimya wenzangu!

Jamani nimekuwa kimya kwa muda sasa. Nilikuwa nakusanya nguvu baada ya igizo la tarehe 14. Wale waliotarajia mabadiliko makubwa nadhani wamekata tamaa. Wengine wanasema bunge limerudia kuwa la chama kimoja. Lakini Frantz Fanon anasema tuendelee kuelimisha wananchi mpaka wajue wao ndio wenye nguvu ya kuleta mabadiliko na hakuna mtu yeyote mmoja anayeweza kuleta mabadiliko ya maana isipokuwa wao wenyewe. Kwa wale wanaokubaliana na kalenda Gregory basi kheri ya mwaka mpya.

9Comments:

At 4:34 PM, Blogger Jeff Msangi said...

Karibu tena Nkya,
Kimya chako kilianza kututisha.Tuendeleee kufanya kinatochotakiwa kufanywa.

 
At 2:02 PM, Blogger Christian Bwaya said...

Nadhani ile ilikuwa tamthilia. Maana inaendelea.
Leo mwongozaji wa tamthilia ametuingiza kwenye hatua nyingine. Wazee ambao tulidhani mchango wao umetutosha, wamerudi tena. Na wanaigiza katika sehemu nyeti kabisa!
Tusubiri kuona kinachoendelea...
Heri ya mwaka mpya kaka.

 
At 4:33 PM, Blogger Ndesanjo Macha said...

Karibu sana Nkya. Igizo lile linaendelea. Huna tiketi ya kuingia ukumbini?

 
At 12:43 PM, Blogger Indya Nkya said...

Wenzangu, kazi tunayo. Wazee sijuhi mpaka lini? Uchifu huu!!!

 
At 7:52 PM, Blogger Ndesanjo Macha said...

Umenunuliwa nini na hawa jamaa wa ari mpya?? Ngoja tutaunda tume ya kuchunguza huu ukimya!

 
At 3:02 PM, Blogger mloyi said...

Frantz Fanon anatupa fundisho kubwa. Tukienzi mafundisho yake tutafika mbali sana. Tuendelee kuwafundisha kwa Njia Mpya mpaka wajitambue.

 
At 4:36 AM, Blogger Ndesanjo Macha said...

Nkya,
ninawasiliana ana Efu Bi Ai ili tuanze kukutafuta.

 
At 7:11 PM, Anonymous Best Survey sites said...

Frantz Fanon anatupa fundisho kubwa.

Cheers,
best survey sites

 
At 4:06 PM, Anonymous What Is Debt Consolidation said...

Wazee sijuhi mpaka lini? Uchifu huu..

Cheers,
what is debt consolidation

 

Post a Comment

<< Home

KITABU CHA WAGENI