Wednesday, June 08, 2005

Wanablogu wa Tanzania na Habari za Siasa

Nakumbuka siku za nyuma kidogo Msangi alitoa changamoto kujadili mapendekezo ya mwanazuoni mmoja aliyeonyesha wasiwasi wake kwamba wengi wa wanablogu Tanzania ni waandishi wa habari na pia hupendelea kuandika habari za siasa. Hili la la waandishi wengi kuwa pia wanablogu nitalijadili kwa kirefu wakati mwingine. Nitalihusisha na tabia ya kutafuta habari kwa watanzania. Kuhusu siasa ni kweli kwamba wengi hujadili habari za siasa. Kwa mtazamo wangu ni kwamba mfumo wa siasa wa nchi au siasa zilizopo ndizo hutoa picha kamili ya mwenendo mzima wa kila kitu. Kama siasa ni mbovu basi kutakuwa na teknolojia mbovu, kutakuwa na sera mbovu za elimu, elimu itakuwa duni, miundombinu duni. Kama mfumo wa siasa haueleweki hakuna kitakachoeleweka. Sera za uchumi hazitaeleweka. Kwa kifupi hakuna kitakachoeleweka au kufanikiwa kama kuna mfumo mbovu wa siasa. Wakati wa siku za nyuma tulikuwa tunasema ili tuendelee tunahitaji: watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora. Unaweza kuwa na watu, ardhi lakini ukakosa siasa safi. Kutakuwa hakuna maendeleo. Siasa safi na uongozi bora vinaendana sana kama una siasa mbovu utakuwa na viongozi wabovu. Huu ndio ukweli. Napenda kuamini kwamba wanablogu wengi wa Tanzania wamegundua hili, na wanajua kabisa siasa zilizopo ni mbovu na ndio maana leo utasikia mtu akisema ni lazima tukitaka tuendelee tusitegemee wafadhili, kesho mtu huyo huyo anasema hatuwezi kuendelea bila msaada wa wahisani. Huku ndiko kukosa mwelekeo wa siasa. Nadhani waandishi wanaona umuhimu wa kuwa na siasa safi kwanza halafu mengine yatakuja tuu. Najiandaa kumwandikia yule bwana mawazo yangu kwa kirefu. Mjadala uendelee.

0Comments:

Post a Comment

<< Home

KITABU CHA WAGENI