Wednesday, June 08, 2005

Afrika na Mikakati ya kuisaidia

Kama kuna bara la majaribio basi ni Afrika. Katika kipindi cha miaka mitano tumesikia mambo kibao ya kusaidi umasikini Afrika; Mara HIPC, Mara Millenium Account Fund, Mara tume ya Blair, mara sijuhi Clinton Fund za UKIMWI mara Bush initiative. Huku kuna mikakati kibao kwa upande wa Afrika lakini yote pia inategeme wafadhili. Sijuhi haya majaribio yatazaa matunda. Sasa hivi Blair na Bush wanajadili pia kuhusu madeni na misada Afrika. Inasemekana watafikia makubaliano karibuni kuhusu kusamehewa madeni lakini kwa masharti fulani. Nakuapia kutakuwa hakuna jipya watakalokubaliana hii ni danganya toto tuu. Tutaambiwa madeni yatasamehewa baada ya masharti kibao kutimizwa. Kuna jipya katika hili? Wasichoonge ni kwamba hayo madeni tunayoambiwa yatafutwa yalitumikaje kwa faida ya walengwa wa Afrika. Utakuta asilimia 60 ya fedha zenyewe zilitafunwa na watu wao halafu tumeshalipa kama mara tatu ya tulivyopewa. Nakuambia kama kuna kufa ndiko huku.

0Comments:

Post a Comment

<< Home

KITABU CHA WAGENI