Monday, October 03, 2005

Bakteria na vidonda vya tumbo

Tofauti na ilivyozoeleka na kuaminika siku zote kwamba vidonda vya tumbo husababishwa kwa kiwango kikubwa na mifumo ya maisha na mfadhaiko(stress), sasa wataalam wamegundua kumbe zaidi ya asilimia zaidi ya asilimia 80 husababishwa na bacteria waitwao "Helicobacter pylori". Wanasayansi wawili toka Australia Barry J. Marshall na J. Robin Warren wamepata tuzo ya Nobel kwa ugunduzi huu. Soma mwenyewe habarii hiyo hapa. Wiki hii pia washindi wengine wa tuzo za Nobeli wa Amani, Kemia, Fizikia watatangazwa. Jumatatu ya tarehe 10/10 ndio atatangazwa mshindi wa nishani hiyo katika uchumi, huku tarehe kamili kwa mshindi katika fasihi ikiwa haijatolewa rasmi. Unaweza kusoma zaidi habari za tuzo za Nobeli hapa

0Comments:

Post a Comment

<< Home

KITABU CHA WAGENI