Thursday, September 22, 2005

Elimu na Kujifunza

Tarehe 25/08/2005 Chuo Kikuu cha Western Cape kiliandaa mhadhara wa kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere. Hili ni tukio la kila mwaka kukumbuka mchango wa Mwalimu katika Elimu. Mwaka huu mzungumzaji alikuwa Dr. Rosa Maria Torres Waziri wa Zamani wa Elimu Nchini Ecuador. Mama huyu alitofautisha kati ya kupata elimu na kujifunza. Baadhi ya mambo aliyosisitiza ni pamoja na: kumaliza mtaala si sawa na kujifunza, kujifunza hakuanzii darasani, kutojua kusoma na kuandika hakumaanishi ujinga, kujifunza si kusoma vitabu tuu, Elimu si kuongeza idadi ya wanafunzi pamoja na mengine mengi. Huu ulikuwa mhadhara mzuri na wa kufurahisha.

0Comments:

Post a Comment

<< Home

KITABU CHA WAGENI