Monday, September 19, 2005

Filamu Mpya ya Kiswahili kuhusu UKIMWI

Nimepata taarifa kwamba Filamu mpya ya Kiswahili iliyotengenezwa Marekani iitwayo TUSAMEHE kuhusu UKIMWI inatarajia kutoka hivi karibuni. Itatoka rasmi mwezi ujayo huko Washinton D.C. na baadaye itaonekana nchi zote za Afrika Mashariki. Cha kufurahisha zaidi ni kwamba kati ya waliocheza sinema hiyo watu Saba ni wazungumzaji wa Kiswahili -watano toka Tanzania na wawili toka Kenya. Cha muhimu ni kwamba kilichowaunganisha wote hawa ni lugha ya Kiswahili. Kampuni iliyoandaa filamu hii pia imekwishatoa filamu nyingine iitwayo Bongoland ambayo inaendelea kuuzwa sehemu mbalimbali duniani.
Nadhani Filamu hii imekuja katika wakati muafaka kwa sababu mbili kubwa; kwanza tatizo la UKIMWI ambalo linazidi kukua na athari zake kuwa mbaya kila ukicha, na pili matumizi ya lugha tamu ya Kiswahili. Uwe tayari kwa filamu hiyo ambayo nataraji itakuwa nzuri na ya manufaa kwetu. Unaweza kusoma zaidi kuhusu Filamu hiyo HAPA

0Comments:

Post a Comment

<< Home

KITABU CHA WAGENI