Tuesday, September 13, 2005

Vitabu

Kuna vitabu viwili nitamshauri kila mtu avisome. Mimi nimevisoma vyote, na uzuri vinavutia kusoma na si virefu sana. Cha kwanza kinaitwa Pambazuko Gizani; kimeandikwa na Kalumuna Mboneko. Usithubutu kukikosa. Kimeandikwa kama riwaya lakini ukikisoma utajionea mwenyewe ukweli wa mambo yanayoelezewa humo ndani. Kwa maoni yangu ni kitabu cha kusomwa na kila mtu. Cha pili ni Rai ya Jenerali; kimeandikwa na Jenerali Ulimwengu. Huu ni mkusanyiko wa makala zake alizokuwa akiandika kwenye gazeti la Rai kuanzia 1993 hadi 1995. Makala hizi japo ni za miaka ya nyuma bado ni mbichi utadhani zimeandikwa leo. Tafuta ukisome. Hutajuata kukisoma. Bei zake nadhani ni za kawaida. Pambazuko Gizani ni shilingi 3,000 na Rai ya Jenerali ni 5,000.

0Comments:

Post a Comment

<< Home

KITABU CHA WAGENI