Monday, August 01, 2005

Tutamkumbuka Daktari Garang

Daktari John Garang, makamu wa rais wa Sudan kwa wiki tatu tuu na kiongozi wa Sudan ya Kusini kwa miaka lukuki emefariki wakati ambapo dunia ilikuwa na matumain makubwa sana kwake hasa baada ya kusaini makubaliano ya amani na serikali ya Khartom. Soma habari hii hapa. Garang, Daktari mchumi aliyewahi kusoma Chuo Kikuu cha Dar-es-Salaam miaka ya nyuma na kupata shahada yake ya udaktari wa falsafa katika chuo hiki hapa alijitolea kupigania haki za wasudani kusini ambao walikuwa wakitengwa na mfumo wa utawala wa Khartom. Kifo chake kitakuwa pigo kubwa kabisa hasa ikitiliwa maanani mkataba wa amani wa hivi karibuni. Alale pema Daktari Garang.

0Comments:

Post a Comment

<< Home

KITABU CHA WAGENI