Saturday, July 16, 2005

Ugaidi

Kwa nini hawa watu wanaoitwa magaidi watoke Misri, Saudi Arabia, Pakistan na nchi nyingine zenye uhusiano mzuri na Marekani na Uingereza? Kwa nini hawatoki nchi kama Iran au Iraq(kabla ya kuvamiwa)? Hili jambo limekuwa likinitatiza mno lakini naanza sasa kupata Mwanga. Huu urafiki wa baadhi ya nchi za kiarabu na nchi za magharibi hauungwi mkono na watu, ni urafiki wa viongozi hivyo wanajaribu kuonyesha hisia zao kwa njia hizi ambazo nchi za magharibi zinaita ugaidi. Lakini kuvamia Iraq na kuua hovyo si ugaid hata kidogo, ni ukombozi. Kabla ya kuvamiwa Iraq kulikuwa hakuna kitu kama watoa maisha mhanga. Naam, sasa wamezalishwa wa kutosha. Kulikuwa hakuna ushahidi wowote wa Alkaida na Iraq. Naam sasa wana tawi kabisa. Kwa vile wanataka Iraq iwe na uhusiano na nchi za magharibi sasa wananchi hawataki wanaonyesha kwa vitendo kama vya kujitolea mhanga, hali ambayo haikuwepo siku za nyuma.
Kwa wale wasikilizaji wa BBC nadhani mmesikai mjadala alioendesha Tido Mhando katika kipindi cha wiki hii- Jumamosi, tarehe 16/07/2005, mmoja wa washiriki wa mjadala ameongea jambo la msingi sana. Kwamba ni waafrika wangapi wanakufa kwa kuchinjwa, wanakufaa kwa njaa, magonjwa yanayotibika nakadhalika kila leo? Hakuna tofauti kati ya mweupe na mweusi katika vifo. Lakini wakifa weupe nakuambia ni kama wao wana haki zaidi. Hawastahili kufa. Mabomu ya London yaliyoua watu 54 hadi sasa yameonyesha hili. Viongozi mbalimbali wanatia saini vitabu vya maombolezo. Inatakiwa sasa kila asubuhi baadhi ya viongozi wakiamka asubuhi jambo la kwanza liwe ni kutia saini vitabu vya maombolezo kwa makumi ya watu wao waliohujumiwa maisha yao kwa Malaria, Kipindupindu, Ajali nakadhalika. Wasisahau pia kutia saini vitabu vya maombolezo kwa wananchi wa Iraq wanaouwa kila siku bila hatia.

2Comments:

At 2:14 PM, Anonymous Mary said...

Jambo la ugaidi limekita mizizi. Tafadhali jihadharini.

 
At 2:16 PM, Anonymous Mary said...

Jambo hili limekuwa kidonda zugu, watu wengi waangamia.

 

Post a Comment

<< Home

KITABU CHA WAGENI