Sunday, July 03, 2005

Angalia hii habari ya huyu Balozi wa Iraq

Habari hii hapa inaonyesha jinsi huyu balozi wa Iraq katika Umoja wa Mataifa alivyo mbinafsi. Analalamika kuuwa kwa binamu yake ambaye anadai hakuwa na hatia. Hivi ni maelfu mangapi ya wairaq wasio na hatia wanaouwa na jeshi la Marekani? Ameumwa sana na binamu yake anasahau kila mwiraq ambaye mtoto, mzazi au ndugu yeyote aliyeuwa ana machungu kama yake ila hawana pa kulalamikia kama yeye. Yeye kama mwakilishi ingebidi aongelee mfumo mzima wa utendaji wa jeshi la wavamizi wa marekani wanavyoua watu hovyo. Sasa kaona binamu yake ni binadamu zaidi kuliko wengine!

0Comments:

Post a Comment

<< Home

KITABU CHA WAGENI