Tuesday, June 28, 2005

Imetokea Karibuni

Dunia hii ina vituko nakuambia. Nilipoambiwa habari hii ya kusikitisha na kufurahisha niligundua binadamu wana mambo si kidogo. Ilikuwa hivi: jamaa mmoja mweupe nina maana mzungu, alikuwa akisafiri toka mji mmoja uitwao Gobabis kuelekea Windhoek huko Namibia akifuatana na mbwa wake na mfanyakazi wa kiume. Kwa vile alikuwa na gari aina ya pick-up, aliamua kukaa na mbwa wake mbele na jamaa akakaa nyuma huku akitwangwa na upepo usio na mfano. Kuepuka kuchapwa sana na upepo ilibidi atizame upande gari linakotokea , kwa wale wazoefu wa kusafiri kwenye magari ya wazi wanajua hii ndiyo njia ya kupunguza kuchapwa na upepo. Jamaa akachochea gari lake, kabla ya kufika walipokuwa wakienda wakapata ajali mbaya, yule mzungu akafa palepale, mfanyakazi na mbwa wakapata majeraha madogo sana. Polisi walipofika kusaidia na kupima ajali wakawa wanamuuliza yule mfanyakazi: hebu tuambie ajali ilivyotokea, jamaa nadhani hakuwa na subira wala hakupepesa macho akawaambia polisi muulize huyo- huku akimnyoshea kidole mbwa. Akaendelea: mimi nilikuwa nikiangalia gari linapotokea kwa sababu ya upepo, marehemu na huyu mbwa ndio waliokuwa wakiangalia gari linapoelekea hivyo walijua kilichotokea. Kwa hivyo mbwa anaweza kuwaelezea vizuri zaidi. Nakuambia polisi hawakuwa na na hamu hata kidogo. Naambiwa mbwa pia alikuwa akilalama kumona tajiri yake akiwa amelala usingizi wa moja kwa moja.

0Comments:

Post a Comment

<< Home

KITABU CHA WAGENI