Tuesday, June 28, 2005

Mchakato wa kuwapata wagombea urais

Nilidhani hii hoja sasa basi, lakini kuna watu wameniuliza naonaje mchakato mzima wa vyama vyote vya siasa kuwapata wagombea urais. Mimi sina ugomvi na mchakato mzima unaotumika najua hizo ni taratibu ambazo vyama vimejiwekea na kukubalika. Ugomvi wangu ni watu wanaoshiriki katika zoezi zima la kuwateua wagombea. Nina maana wajumbe wa Halmashauri Kuu na Mkutano Mkuu wa vyama. Je wajumbe hawa wanaofanya maamuzi mazito namna hii wana uelewa gani wa mambo. Hivi kwa mfano ni wangapi wana uelewa wa rais anayetakiwa katika kipindi hiki cha mageuzi mazito na ushenzi unaofanywa na mataifa makubwa kwa nchi changa? Ni wajumbe wangapi wanaoelewa hali halisi au ni wafuata mkumbo tuu? Hivi wajumbe hupatikana kwa vigezo gani? Ni ualiwatani wa vijiweni, uimbaji wa kutukuza vyama au kupandisha bendera za vyama kwenye magenge au biashara? Hawa wajumbe wanafanya maamuzi makubwa sana. Wanajadili taarifa za utekelezaji wa kazi za serikali, wanatoa maagizo kwa serikali, wanateua wagombea urais nakadhalika. Hivyo wajumbe hawa wanatakiwa wawe waelewa kweli kweli si ualiwatani. Ni lazima vigezo viwekwe kwa wanaogombea nafasi katika ngazi hizi za halmashauri kuu na mkutano mkuu kwa vyama vyote la sivyo tutaona maajabu.

0Comments:

Post a Comment

<< Home

KITABU CHA WAGENI