Thursday, June 30, 2005

Mambo ya UKIMWI yapamba moto

Jamani haya mambo ya UKIMWI yanakuwa sasa ni siasa. Kama mtakumbuka siku za nyuma niliandika jinsi Daktari anayetangaza matumizi ya vitamini kama njia ya kusaidi kupunguza madhara ya UKIMWI anavyobanwa. Nimeandika pia kwenya makala yangu ndefu iliyopo ndani ya blogu sasa. Basi siku za Karibuni Waziri wa Afya wa Afrika ya Kusini, Manto Tshabalala- Msimang alionana na huyo Dr. Rath (bingwa wa vitamini) na anaelekea anakubaliana na hoja kwamba vitamini kiasi fulani zina manufaa katika kumsaidia mhathirika. Baada ya hapo akatoa tamko kwamba wananchi wawe na uchaguzi wa dawa zilizopo, wale wanaoweza kupata ARVs waendelee nazo wale wa vitamini na dawa asilia waachwe wachague kwa sababu asilimia 80% ya wagonjwa wanaofika hospitali za serikali huwa wanatembelea waganga wa asili kwanza. Wabunge wa chama cha wazungu cha DA wamekuja juu, sasa wanataka kumshitaki katika baraza la maadili la watoa huduma za afya kwa kuwaambia wanachi wanaweza kuchagua dawa ambazo hazijathibitishwa kutibu kitaalam. Kuna mvutano usio wa kawaida kati ya watetea kampuni za dawa za magharibi na watetezi wa dawa asilia na vitamini. Huu ukasuku wa waafrika kufikiri kila kitu lazima kipitishwe na wazungu utatumaliza. Huyu Waziri ni ngangari sana na si mhumini mzuri sana wa nadharia za UKIMWI zilizoenezwa na nchi za magharibi ambazo kwanza hazina uthibitisho wa kitaalam. Rais Thabo Mbeki pia alikuwa mmoja wa watu waliokuwa wakihoji nadharia ya HIV-UKIMWI. Ukienda kwenye tovuti hii utakumbana na picha yake pamoja na mambo mengi yahusuyo UKIMWI

0Comments:

Post a Comment

<< Home

KITABU CHA WAGENI