Sunday, October 23, 2005

Dawa za ARVs husababisha magonjwa ya moyo

Kuna habari hii hapa inayosema kwamba dawa za kurefusha maisha husababisha magonjwa ya moyo. Tafadhali isome. wakati fulani kwenye blogu yangu ya kiingereza niliandika kuhusu hili jambo nikijenga hoja kwamba wale walioshtaki kampuni iliyokuwa ikitengeneza dawa za kutuliza maumivu ziitwazo VIOXX na baada ya kuzitumia mgonjwa magonjwa ya moyo hawakuwa wajinga na inawezekana kabisa kwamba kampuni hizi zinazotengeneza ARVs baadaye zikashtakiwa. Jamaa mmoja kanijia juu kishenzi. Lakini ukweli wa mambo ni kwamba dawa hizi zina madahara makubwa sana katika mwili.

0Comments:

Post a Comment

<< Home

KITABU CHA WAGENI